Pwani FM: #KenyaNiMimi itainua maisha ya vijana – Asema Nadia Abdalla

Katibu Mwandamizi katika Wizara ya Mawasiliano, Teknoljia, Uvumbuzi na Maswala ya Vijana Nadia Ahmed Abdalla amehimiza kuwa vuguvugu la #KenyaNiMimi itainua maisha ya vijana. Aliongeza kuwa vijana wajitokeze, wafahamishwe zaidi na kunufaika kutokana na mipango/miradi mingi ya serikali kama Ajira Digital, KBC Studio Mashinani, Mikopo na mengineo.
Nadia alihojiwa Ijumaa tarehe 27 Novemba, 2020 na Mwanahabari wa Pwani FM Fundi Bengo.